Siku ya leo tutaendelea na kwa kuangalia magonjwa mengine ya kuku ambayo hutibika kwa dawa kama ifuatayo:
Ugonjwa huu husababishwa na virusi.
Dalili.
Kuku huzubaa na kujikunyata
Kuku kuharisha kinyesi chenye damu au kinyesi cha kahawia
Kuku hudhoofika,manyoya huvurugika na kulegea mabawa na kuonekana kama wawevaa koti
Kuku hupungukiwa homa ya kula
Vifo huwa vingi kwa vifaranga
Tiba ya ugonjwa huu.Wape kuku wako dawa kama Esb 3, Amprolium, au Basulfa.
Kinga za ugonjwa huu.Zingatia usafi wa banda la kuku na usiruhusu unyevuunyevu katika banda la kuku.
Dalili za ugonjwa huu ni;
Kuku hupata homa kali
Kuku huarisha kinyesi cha kijani au njano
Vifo huwa vingi hasa kwa vifaranga wenye wiki 1-2
Kuku huzubaa,kuvimba viungo vya miguu,kuchechemea,kukosa hamu ya kula
Kuku wanaotaga hupunguza utagaji,hutaga mayai yenye ganda laini na hupata vifo vya ghafla
Tiba za ugonjwa huu.
Dawa za oxytetracycline kama Furamax,Typhoprim hutibu ugonjwa huu.
Dawa za oxytetracycline kama Furamax,Typhoprim hutibu ugonjwa huu.
Kinga za ugonjwa huu.
Hakikisha usafi wa banda na vyombo vya chakula na maji kwa kuku.
Tenganisha kuku wagonjwa na wazima
Hakikisha usafi wa banda na vyombo vya chakula na maji kwa kuku.
Tenganisha kuku wagonjwa na wazima
3. MINYOO
Hushambulia kuku wote wakubwa na vifaranga
Hushambulia kuku wote wakubwa na vifaranga
Dalili za ugonjwa huu
Kuku hukonda
Kuku huarisha
Kuku hukohoa
Kuku hupunguza utagaji
Kuku hudumaa katika ukuaji/hawakui vizuri
Kuku hupungua uzito
Tiba za ugonjwa huu.
Tumia dawa za minyoo kama piperazine
Tumia dawa za minyoo kama piperazine
Kinga za ugonjwa huu.
Wapewe dawa za minyoo mara kwa mara kila baada ya miezi mitatu
4.VIROBOTO/CHAWA/UTITIRI
Hushambulia sana vifaranga na hutokea vifo kwa wingi kwa vifaranga Kwa kuku wakubwa tatizo halionekani kwa sana lakini nao huathiriwa sana.
Hushambulia sana vifaranga na hutokea vifo kwa wingi kwa vifaranga Kwa kuku wakubwa tatizo halionekani kwa sana lakini nao huathiriwa sana.
Dalili za ugonjwa huu.
Kuku kutochangamka
Ukuaji mdogo wa kuku
Kuku kutotaga na kuhatamia vizuri kutokana na kusumbuliwa na chawa,utitiri au viroboto
Viroboto huonekana kuganda machoni wakinyonya damu
Tiba za ugonjwa huu
Tumia dawa za unga kama sevin dust 5% ,Malathion ,akheri powder kwa kuku wote na mabanda yao.
Tumia dawa za unga kama sevin dust 5% ,Malathion ,akheri powder kwa kuku wote na mabanda yao.
Kinga za ugonjwa huu.
Boresha usafi wa mabanda ya kuku.
..........................................................................
0 comments:
Post a Comment