script>" " ".

Get our Android App in Playstore DOWNLOAD HERE!

X





https://www.mshindoveterinarycentre.com/ 
Utangulizi
Ufugaji wa kuku wa kienyeji kwenye nchi zinazoendelea hususan Tanzania na Afrika kwa ujumla umekuwa ni wa mazoea. Wafugaji wameshindwa kugeuza mradi huu kuwa biashara na kujiongezea kipato cha kaya zao. Hii imetokana na ukosefu wa elimu ya ufugaji, ukosefu wa mabanda bora, uwepo wa magonjwa mbalimbali kama mdondo na ndui, pia upatikanaji haba wa chanjo za magonjwa.
ufugaji kuku
Matokeo yake yamekuwa ni upatikanaji haba wa mazao yatokanayo na kuku.
Mambo ya kuzingatia katika banda.
* Banda liwe na urefu wa kutosha kumuwezesha mfugaji kuingia ki urahisi na kufanya usafi.
* Banda lijengwe mahali pasipotuamisha maji au madimbwi ya mbu.
* Banda liwe na madirisha ya kutosha yanayopitisha mwanga na hewa
* Weka pumba za mpunga au maranda bandani kiasi cha sentimeta 4-6
* Gawa vyumba katika banda lako ambapo kuwe na maeneo ya kutotolea vifaranga na chumba cha majike yanayotaka kuatamia.
* Ching'wekwe(umbo dogo)
* Singamagazi ( hupatikana Tabora)
* Mbeya
* Pemba
* Unguja
* Kishingo
Newcastle(kideli)
Huu ni ugonjwa unaosababishwa na virusi. Dalili zake ni kuharisha choo cha kijani na njano, kukohoa na kupumua kwa shida, kukosa hamu ya kula , kutoa kamasi na machozi
Kinga ya ugonjwa huu ni newcastle vaccine kwa utaratibu wa siku 3, wiki 3 na miezi 3.
Minyoo
Minyoo kama chango na tegu huathiri kuku wa kienyeji. Kuku hukosa hamu ya kula na mayai hupungua. Mchanganyiko wa dawa tatu hutumika kuangamiza minyoo, dawa hizi ni nipiperazine,phenothiazine, na butynorate. Dawa hizi ziko katika mfumo wa vidonge, tumia kidonge 1 kwa kuku mzima na nusu kwa vifaranga.
Magonjwa ya mapafu
Magonjwa haya huathiri mfumo wa hewa na kuambatana na mate na sauti kama kikohozi. Dalili zake ni vidonda vyenye utando wa kahawia usoni na chini ya midomo, kukosa hamu ya kula na vifo vingi.
Kinga yake ni kuchanja vifaranga vikiwa na umri wa mwezi 1-2 kwa kutumia chanjo ya fowl pox vaccine
Ni muhimu mfugaji akawapa kuku wake vitamin A, kwani upungufu wa vitamin A huathiri zaidi kuku wadogo na wanaokua na mara nyingi hupelekea vifo 
* Hutupatia fedha kwa kuuza nyama na mayai
* Mayai yana madini muhimu kama methionine na cystine ambayo ni muhimu kwa watoto wachanga
* Kinyesi cha kuku ni mbolea kwa matumizi ya shambani
* Kiwanda asili cha kutotolesha vifaranga badala ya incubators ambazo ni gharama kubwa
* Manyoya ya kuku hutumika kutengeneza mapambo mbalimbali, mito na magodoro

.......................................................................................................................................................

0 comments:

 
Top