
MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA KABLA YA KUANZA KUFUGA NG’OMBE WA MAZIWA
: Kwa kawaida unapotaka kufuga ng’ombe wa maziwa unakuwa na malengo mawili makubwa yafuatayo:
• Kama unazo nyenzo muhimu kwa ufugaji huo.
• Jinsi ya kuanza kufuga.
• Kuwa na shauku ya kutaka kujifunza wakati wote na kuwa na mwamko wa kibiashara:
• Epukana na kujiamini sana na kuwa na matarajio yasiyowezekana, hasa katika viwango vya uzalishaji, bei ya maziwa, faida kubwa. Haya yanaweza kukukatisha tamaa mapema!
• Ng’ombe mzuri kwa kutoa maziwa
• Majengo na zana zinazostahili.
• Mapendezo ya mfugaji mwenyewe
• Mtaji na nyenzo alizo nazo mfugaji
• Mfumo wa masoko
(c) The American Guernsey Cattle Club; 70 Main st. Peterborough, New Hampshire 03458. Journal- THE GUERNSEY BREEDERS JOURNAL.
Katika aina hii, mfugaji huweka makoo na ndama wote wanaozalishwa kwa ajili ya kukuzwa ili wawe mitamba ya kubadilisha na makoo walio wazee, wenye kutoa maziwa kidogo na wenye matatizo mbalimbali. Faida ya mfumo huu ni pale mfugaji anapokuwa na uwezo wa kukuza mitamba mizuri yeye mwenyewe na kuweza kuitumia kuendeleza na kuongeza uzalishaji wa maziwa. Tatizo kubwa ni mahitaji ya ziada ya chakula ndama hadi anapokuwa mtamba.
Mfugaji kuzalisha mwenyewe chakula chote (hasa nyasi) kinachohitajika. Faida kubwa ya aina hii ya ufugaji ni uhakika wa kuwa na chakula bora (forage) kwa ajili ya mifugo wakati wote. Vilevile, kama mfugaji anatumia mbinu bora za kilimo, basi gharama huwa ndogo sana katika uzalishaji wa nyasi na majani.
Mapungufu makubwa ya mfugaji kuzalisha chakula mwenyewe ni mahitaji makubwa ya mtaji wa kuanza kwa ajili ya ardhi ya kutosha, zana huduma ya wataalam na malipo ya vibarua. Wakati mwingine ardhi inaweza kuwa taabu kupatikana.
Ufugaji wa aina hii ndiyo mara nyingi unapendekezwa kwani hutoa matumaini ya mafanikio. Kwa wafugaji wenye ng’ombe kidogo (5-10), hushauriwa kutumia kilimo mseto ili kuweza kutumia mabaki ya shambani kulishia mifugo.
Mfumo huu ulifanikiwa sana kule Zanzibar katika miaka ya 80 kwa msaada wa programu ya chakula duniani (World Food Program)
MFUGAJI HUNUNUA CHAKULA CHOTE KINACHOHITAJIKA KWA MIFUGO
Mfumo huu huondoa yale mahitaji makubwa ya kifedha wakati wa kuanza, pamoja na kupunguza muda unaohitajika kwa uzalishaji na utunzaji wa malisho.
Hata hivyo mapungufu yake mara nyingi ni kule kutopata malisho ya kutosheleza na yaliyo bora. Vilevile gharama ya ununuzi na usafi rishaji mara nyingi kujiandaa vizuri.
VIPI UANZE
Kuna aina nyingi za kuanzia, lakini la msingi ni kujiandaa vizuri. Katika sifa, mfugaji anahimizwa kuwa awe anahamasika, awe mvumilivu, mchapakazi na aweze kuzikubali hasara zinapotokezea.
Katika kupanga, lazima mfugaji awe na makisio yanayokubalika. Asiwe na pupa katika suala la mikopo ya kuendeleza mifugo, malisho, uzalishaji, uzazi, afya na kadhalika. Vilevile anapaswa kuwa na bajeti ya kila mwaka. Mfugaji anapaswa kupanga matumizi ya mtaji kwa mujibu wa umuhimu kama;-
• Ununuzi wa ng’ombe wenye kutoa maziwa kwa wingi.
Kupata mchango wa kifamilia au vyama vya kuweka na kukopa. Kama umekusudia kudumu katika ufugaji, unaweza kutumika mtaji mdogo ulio nao kununulia nyenzo muhimu na kukodi nyenzo nyingine hadi ufi kie lengo ulilolikusudia.
Zingatia kwa makini somo hili kisha jadili yafuatayo:-
• Kama wewe ni mfugaji tayari, unafi kiri ni jambo gani lingefaa kutangulia kati ya kujijengea sifa za kuwa mfugaji, au kuwa na mtaji wa kununulia nyenzo muhimu zinazokubalika? Kwa nini?
• Ni matatizo yapi yanayokukabili katika ufugaji wa ng’ombe wa maziwa? Yataje pia pendekeza njia za kuyatatua
Mfumo huu huondoa yale mahitaji makubwa ya kifedha wakati wa kuanza, pamoja na kupunguza muda unaohitajika kwa uzalishaji na utunzaji wa malisho.
• Ununuzi wa ardhi kwa ajili ya malisho
• Kugharamia mfumo wa mauzo ya maziwa
• Ununuzi wa zana na vifaa vinavyotakiwa.
Njia za kumpatia fedha za mtaji zinaweza kutokana na kukusanya akiba polepole kutokana na kazi nyingine, kukopa baada ya kutayarisha mchanganuo unaokubalika.
....................................................................................................................................................................
0 comments:
Post a Comment