script>" " ".

Get our Android App in Playstore DOWNLOAD HERE!

X




UNAFAHAMU NINI MAANA HALISI YA UFUGAJI WA SAMAKI.


Hili ni swali la msingi kabisa kufahamu ili ikusaidie kufahamu kitu unachotaka kutekeleza.
Ufugaji wa samaki ni kazi ya kupanda,kukuza na kutunza samaki katika bwawa au uzio (uliotengenezwa kwa vyuma,miti pamoja na nyavu) au eneo lolote ambao uthibiti wake uko chini ya mamlaka ya mfugaji mwenyewe.Mabwawa yanaweza yakawa ya kuchimbwa na watu(japo kuwa mabwawa ya asili pia yanaweza kufugia samaki) wakati yale yanaweza yakawekwa katika eneo lolote lenye maji mengi kama vile ya ziwa,mto au bahari.
Ufugaji wa samaki katika kiasi Fulani si sawa na ukuaji wa samaki katika mito,maziwa na bahari.Tofauti kubwa iliyopo samaki wanaofugwa na wasiofugwa ipo katika huduma,huduma wanazopata samaki wanaofugwa huwekwa kwa idadi maalumu ndani ya bwawa,kupatiwa chakula na kuhudumiwa vizuri.
Ufugaji wa samaki sio kitu kipya kabisa hapa Tanzania,baadhi ya watu wamekuwa wakifuga samaki kabla ya hata kupatikana kwa uhuru wa Tanganyika.Lakini baadhi ya wafugaji wamekuwa wakitoa matunzo hafifu kwa samaki hao,hivyo kupelekea mavuno hafifu katika ufugaji huo.kwa miaka ya hivi karibuni serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania imekuwa ikitilia mkazo katika utoaji wa elimu (ugani) ili kuboresha mafanikio yake yaweze kupatikana kama nchini nyingine zinazotekeleza miradi hii.Kupitia muongozo wa mafunzo haya kila mtu atafahamu faida ya ufugaji na namna ya kuwafuga samaki wake ili waweze kukua vizuri na kumletea tija katika shughuli hiyo,na pia kuwa ni sehemu ya ajira hasa kwa vijana wazee walio katika umri wa kuustaafu hali itakayo wasaidia kujiingizia kipato na kuishi bila shaka yeyote ya kipato.
Kwa sasa samaki ambao hufugwa zaidi katika maji baridi (maji yasiyo ya chumvi) ambayo vyanzo vyake ni kama vile ya ziwa,mto,chemichemi ,kisima ya bomba,ni sato/pelage (Tilapia) na kambale (catfish).Kwa upande wa samaki wanaofugwa Zaidi katika maji chumvi(bahari) ni mwatiko/mkuyuyu (milk fish) na Kamba (prawns).
...................................................................................

0 comments:

 
Top